Ijumaa, 1 Februari 2019

TAARIFA KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI

Kaimu Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali anapenda kuyakumbusha Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini kuwasilisha Taarifa za mwaka 2018 kwa mujibu wa kifungu Na. 29 (a) & (b) cha Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 na Kanuni Na. 10 ya Kanuni za Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2004 (GN 152, 2004) kama ilivyorekebishwa na Kanuni Na. 6 ya Kanuni za Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2014 (GN 8, 2015), kabla ya tarehe 15 Aprili, 2019. Taarifa hiyo ijumuishe Taarifa za utendaji kazi, Taarifa za fedha zilizokaguliwa, NGO Fomu Na. 10 na malipo ya ada ya mwaka. Mashirika yatakayoshindwa kutekeleza agizo hili ndani ya kipindi husika, yatachukuliwa hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kutozwa faini.

Kauli mbiu yetu

BUFADESO kwa maendeleo ya wakulima

MUHIMU

Makala na picha zinazochapishwa katika blogu hii ni kwa ajili ya taarifa na kumbukumbu za Shirika la Bunda Farmers Development Support Organization (BUFADESO)
Hairuhusiwi kutumia yaliyomo katika blogu hii (HASA PICHA) kwa shughuli zozote bila ruhusa ya mmiliki wa blogu hii ambaye ni BUFADESO