Ijumaa, 16 Novemba 2018

Kongamano la Mwaka kwa Wadau wa Kilimo-Mseto-2018


Vi Agroforestry Tanzania inapenda kuwaalika wadau wote kwenye kongamano la maonesho ya shughuli za kilimo mseto litakalofanyika kuanzia tarehe 22 hadi 24, November. Maonesho yatafanyika katika kituo cha mafunzo ya kilimo kilichopo Bweri katika Manispaa ya Musoma kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni.

Wanaoalikwa kuhudhuria kongamano hilo ni pamoja na vikundi vya wakulima wadogowadogo, makampuni ya uzalishaji na utengenezaji wa bidhaa mbalimbali, makampuni ya mbegu, makampuni yanayo zalisha viuatilifu, taasisi za fedha, taasisi za elimu, viwanda vya nguo, wizara na taasisi za serikali, taasisi za utafiti pamoja na taasisi za afya na bima na wengine wote watakaopata nafasi.

Kongamano hilo litajumuisha maonesho ya tekinolojia mbalimbali za kilimo, huduma na bidhaa za kilimo kwa kuzingatia utaratibu utakaowekwa na waandaaji.

Mazingira endelevu ni agenda ya kudumu ya Taasisi yetu. Katika maonesho hayo pia kutakuwepo na mafunzo mbalimbali yatakayotolewa na wadau na wakulima washiriki yatakayo toa fursa ya kujifunza na kupata maarifa mapya kwa mstakabali mwema wa mazingira yetu na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Tunapenda kuwahahakishia ushirikiano wetu katika mwendelezo wa utoaji wa elimu endelevu, uzoefu, technologia na mawasiliano katika kuhakikisha kilimo na mazingira endelevu vinadumishwa. Ratiba nzima itakolezwa na vikundi kadhaa vya burudani vitakuwepo kutoa burudani.

Kauli mbiu ya maonyesho ya mwaka huu ni “Kilimo Mseto kwa Maendeleo ya Viwanda” zalisha kwa tija kufikia maendeleo endelevu.

Kwa mawasiliano zaidi juu ya kongamano la mwaka huu tafadhali wasiliana na Mratibu wa kongamano kwa kutumia Email james.juma@viagroforestry.org ama namba ya simu 0786-648000/0759070182.


Kauli mbiu yetu

BUFADESO kwa maendeleo ya wakulima

MUHIMU

Makala na picha zinazochapishwa katika blogu hii ni kwa ajili ya taarifa na kumbukumbu za Shirika la Bunda Farmers Development Support Organization (BUFADESO)
Hairuhusiwi kutumia yaliyomo katika blogu hii (HASA PICHA) kwa shughuli zozote bila ruhusa ya mmiliki wa blogu hii ambaye ni BUFADESO