Jumanne, 8 Desemba 2015

Vi AGROFORESTRY yakabidhi shughuli kwa BUFADESO

Mradi wa Vi AGROFORESTRY Kanda ya BUNDA ulioanza rasmi mnamo mwaka 2008 katika ngazi ya vijiji vya tarafa ya Serengeti na Chamuriho. Kata 13 ziliwezeshwa kwa kujengewa uwezo wa mafunzo ya mazingira, kilimo, ujasiriamali, uimarishaji wa vikundi na masuala mtambuka ikiwemo usawa na Jinsia na mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI.
Mwaka 2009 Vi AGROFORESTRY ilibadirisha mfumo wa utendaji toka ngazi za vijiji kwenda ngazi ya kata.
Mbinu zilizotumiwa ni pamoja na

  1. Kutembelea mkulima mmoja mmoja
  2. Kutoa mafunzo mbalimbali kupitia vikundi vya wakulima.
  3. Kutoa elimu kupitia taasisi hasa mashule
  4. kufanya kampeni za uhamasishaji hasa utunzaji wa mazingira
  5. mikutano na hadhara
  6. mashamba darasa.
Shughuli zikitekelezwa na shirika la VI AGROFORESTRY ni pamoja na:-
  • Ujengaji uwezo kwa kuhamasisha uanzishaji, uimarishaji na uendeshwaji wa vikundi ambapo vikundi 437 vilianzishwa.
  • uhamasishaji juu ya matumizi ya mfumo wa kilimo mseto kwa wakulima.
  • Elimu ya mabadiriko ya tabia nchi.
  • ujasiriamali
  • ushawishi na utetezi
  • masuala mtambuka: masuala ya usawa wa kijinsia, UKIMWI na virusi vya Ukimwi
Tarehe 7 Disemba 2015, Shirika la Vi Agroforestry lilifanya mkutano na wadau ikiwemo serikali na kutangazakuwa kuanzia mwaka 2016, shughuli zilizokuwa zinafanywa na shirika la Vi zitakabidhiwa kwa shirika la Wakulima lililoanzishwa na vikundi vya wakulima, wafugaji na wavuvi wilayani Bunda, BUFADESO. Katika mkutano huo, shirika la Vi AGROFORESTRY lilitoa vyeti kwa wawezeshaji jamii wa BUFADESO waliopatiwa na kufuzu mafunzo mbalimbali.
Meneja wa Vi na Mkuu wa kitengo cha Ujengaji wa Ubia katika mkutano

Mtaalamu wa Vi akisoma ripoti ya utekelezaji wa shughuli

Baadhi ya washiriki katika mkutano

Mwenyekiti wa BUFADESO akitoa maelezo

Muwezeshaji Jamii akipokea cheti cha kuhitimu mafunzo kutoka Vi AGROFORESTRY

Muwezeshaji Jamii akipokea cheti


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kauli mbiu yetu

BUFADESO kwa maendeleo ya wakulima

MUHIMU

Makala na picha zinazochapishwa katika blogu hii ni kwa ajili ya taarifa na kumbukumbu za Shirika la Bunda Farmers Development Support Organization (BUFADESO)
Hairuhusiwi kutumia yaliyomo katika blogu hii (HASA PICHA) kwa shughuli zozote bila ruhusa ya mmiliki wa blogu hii ambaye ni BUFADESO