Alhamisi, 20 Oktoba 2016

Kilimo cha Mbaazi

Mazingira ya kustawi
Ni mmea wenye mizizi mirefu kwenda chini, na huweza kuongeza nitrojeni
Huhitaji mazingira ya joto, kuanzia joto 25-40 sentigrade, haipendi baridi hivyo piga vizuri hesabu zako ni ,muda gani unataka kupanda hadi kuvuna. Kwa tanzania hapa maeneo mengi ya sehemu zenye joto yanakubali mazao haya
Ni mimea inayoweza kuchanganywa na ulezi, au mtama na mahindi

Nafasi ya upandaji
MITA 1 KWA 1.5M , KUTOKA MCHE HADI MCHE 1M, NA MSTARI HADI MSTARI 1.5 M, Katikati yake unaweza unaweza kuchanganya na mazao mengine, kama vile maharage, au hata Mahindi

MUDA WA KUOTA MBEGU
Tangu kupanda mbegu hadi kuota huchua siku 4 hadi 21, na baada ya hapo mimea huanza kukua polepole, hivyo hakikisha unazuia magugu

MUDA WA KUKOMAA
Tangu kupanda hadi kutoa maua,huchukua siku 60 hadi 80, na baada ya maua huchukua siku 50-75 kutengeneza mbegu zilizokomaa, hivyo huchukua kati ya miezi 5 hadi 6 kukomaaa

IDADI YA MEBEGU KWA EKA 1
KILO 10 hutosha kwa ekari moja, kama unaweka mbegu mbilimbli kwa shimo, na kilo 5 hutosha kwa ekari moja kama unaweka moja moja kwa shimo

WADUDU WA HARIBIFU
1. Funza wa matunda
2. Funza wa kukata mimea ikiwa michanga
3.Mnyauko (Fusarium Wilt)
5. Ukungu-Fangasi
Madawa ya kuzuia waduu
. 1. Karate 2. Match, 3. Phyrinex, 4. uduall, 5. Seecron, Moja wapo ya hizo dawa zitakusaidia sana, LITA 3 ZA DAWA ZITAKUTOSHA,  

Madawa ya kutumia kuzuia ukungu ni kama vile
1. Ridomil Gold 2. Ebony (Mancozeb +Metalaxyn), 3, Ivory, 4. Nordox etc Moja wapo ya hizo dawa zitakusaidia sana, LITA MBILI /KILO MBILI ZA DAWA ZITAKUTOSHA

MBOLEA ZA KUPANDIA
Wakati wa kupanda, mboleya kama vile Yara Miller Winner, au NPK, DAP, MiNJINGU AU TSP, zitakufaa, angalu mifuko 2 kwa eka 1

WAKATI WA KUKUZIA
Utahitaji mbolea kama vile, CAN, UREA, AU NPK, Au Yara Miller winner, Mifuko 3 itakutosha

MAVUNO
Mavuno kwa eka moja ni kati ya tani 1 hadi 4, yaani ( gunia 10 hadi 40 za uzito wa kilo 100). Hii inategemeana na rutuba ya ardhi katika shamba husika.












 na
Baraka KAMESE
Mratibu-BUFADESO

Kauli mbiu yetu

BUFADESO kwa maendeleo ya wakulima

MUHIMU

Makala na picha zinazochapishwa katika blogu hii ni kwa ajili ya taarifa na kumbukumbu za Shirika la Bunda Farmers Development Support Organization (BUFADESO)
Hairuhusiwi kutumia yaliyomo katika blogu hii (HASA PICHA) kwa shughuli zozote bila ruhusa ya mmiliki wa blogu hii ambaye ni BUFADESO