Jumanne, 5 Juni 2018

LEO NI SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI


Leo ni siku ya MAZINGIRA DUNIANI. Siku ya Mazingira Duniani huazimishwa duniani kote kila mwaka, tarehe 5 mwezi wa Sita. Lengo la siku hii ni
Kauli mbiu ya Kimataifa ya mwaka huu 2018 kidunia inasema “KOMESHA UCHAFUZI WA MAZINGIRA UTOKANAO NA PLASTIKI” Leo la kauli mbiu hii ni kuhamasisha watu wote kuachana na matumizi holela la plastiki yanayosababisha uchafuzi wa mazingira ikiwemo ardhi, hewa na vyanzo vya maji kama maziwa na bahari. Uzalishaji na matumizi ya kupindukia ya vifaa vya plastiki huathiri mazingira na bayoanuai na viumbe akiwemo mwanadamu. Hivyo dunia anahamasishwa kuwa na harakati endelevu za kulinda maisha ya viumbe na maliasili ili kuifanya dunia kuwa safi na yenye mazingira bora kwa kutokuwa na uchafuzi wa hewa, ardhi, na ,maji utokanao na matumizi holela ya vifaa vya plastiki. Kidunia maadhimisho ya siku hii ya Mazingira Duniani yatafanyika nchini India. India imechaguliwa na Umoja wa Kimataifa kutokana na harakati za muda mrefu za nchi hiyo katika kupambana na matumizi holela ya plastiki. Kwa hivi sasa nchi ya India imeonyesha uongozi bora katika kukabili mabadiliko ya tabia nchi na ni nchi yenye mikakati thabiti ya kuhamia kwenye uchumi utoao kiwango kidogo cha hewa ukaa.
Siku ya Mazingira Duniani ilianza kuadhimishwa mwaka 1972 na sasa imekuwa ni maadhimisho ya kimataifa yenye lengo la kuelimisha umma kuhusu masuala mbalimbali yahusuyo mazingira.
Nchini Tanzania Kauli mbiu ya mwaka huu ni “MKAA NI GHARAMA, TUMIA NISHATI MBADALA. Serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka kauli mbiu hii kutokana na kiasi kikubwa cha maeneo ya Misitu yanayoharibiwa kwa ajili ya kupata mkaa. Takwimu zinaonyesha hadi kufikia mwaka jana (2017) kiasi cha hekta 46,942 huharibiwa kila mwaka. Uharibifu wa misitu unasababisha uwepo wa changamoto za kimazingira kama vile ukosefu wa mvua unaoleta ukame;  hali ya jangwa na joto; upotevu wa viumbe hai mbalimbali na mimea ya asili; uharibifu wa vyanzo vya maji na uchafuzi wa ardhi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kauli mbiu yetu

BUFADESO kwa maendeleo ya wakulima

MUHIMU

Makala na picha zinazochapishwa katika blogu hii ni kwa ajili ya taarifa na kumbukumbu za Shirika la Bunda Farmers Development Support Organization (BUFADESO)
Hairuhusiwi kutumia yaliyomo katika blogu hii (HASA PICHA) kwa shughuli zozote bila ruhusa ya mmiliki wa blogu hii ambaye ni BUFADESO