Jumanne, 17 Machi 2020

Ugonjwa wa COVID-19. Hatua za tahadhari zilizochukuliwa na ofisi ya Vi Tanzania


Mwezi wa kwanza (January) 2020, Shirika la afya duniani (WHO) lilitangaza mlipuko wa ugonjwa mpya uliojulikana kwa jina la virusi vya corona. Kwa mara ya kwanza ugonjwa umetokea katika jimbo la Hubei nchini China. Shirika la afya duniani limeutangaza ugonjwa huu kuwatishio kwa afya ya jamii kimataifa. Maeneo yote ya jamii yetu,ambayo ni pamoja na biashara na ajira, lazima kuwa mustari wa mbele kama tuna hitaji kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huu. Leo jumatatu ya tarehe 16 machi, mgonjwa wa kwanza wa COVID-19 ametambuliwa Tanzania katika mkoa wa Arusha.

Mgonjwa wa COVID-19 anapo kohoa au kupiga chafya hutoa majimaji yenye vimelea vya maambukizi. Majimaji haya hudondoka jirani na pia kwenye vitu kama madawati, meza nahata simu ya mkononi.Watu waliopo jirani wanaweza ambukizwa kwa kugusa vitu hivyo. Hiyo ni baada ya kuwa wamegusa macho yao, pua nahata midomo. Kama utakuwa umesimama ndani umbali wa mita moja kutoka alipo mgonjwa wa COVID-19 unawezaambukizwa kwa njia ya hewa. Kwa maana nyingine ugonjwa wa COVID-19 unaambukizwa sawa na ugonjwa wa mafua.Watu wengi waliougua ugonjwa wa COVID-19 wamekuwa na dalili za kawaida/nyepesi na baadaye kupona.

Ofisi ya Vi Agroforestry Tanzania, inachukua hatua zifuatazo:

*         Ikiwa hujisikii vizuri,hata kama una mafua na kikohozi cha kawaida,au homa ya kawaida, tafadhali baki nyumabani, na kama ikiwezekana fanya kazi zako za kiofisi ukiwa nyumbani.Epuka kugusana na mtu au mwanafamilia alie ndani ya umbali wa mita moja, hii ni kulinda usalama wa wengine ili usiwaambukize. Pia kama unashaka kuambukizwa COVID-19 fika hospitali haraka iwezekanavyo.

*         Nawa mikono yako mara kwa mara kwa kutumia sabuni na maji. Ni kwa sababu kunawa mikono huua virusi vya corona vilivyoko mikononi mwako na kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa COVID-19.Kunawa mikono vizuri,tena mara kwa marani njia yenye ufanisi zaidi ya kuzuia kuenea kwa ugonjwa huu,zaidi ya matumizi ya kemikaliza kwa kusafisha mikono. Epuka kugusa macho yako, pua na mdomo kwa mikono isiyo safi.


*         Walakini, sabuni ya kunawa mikono yenye 60% alcohol itakuwepo getini mwa ofisi za Vi Agroforestry, kwa ajili ya wafanyakazi na wageni kunawa mikono yao kabla ya kuingia ofisini. Pia sabuni hizo zitakuwepo ndani ya ofisi.

*         Tutahakikisha mazingira yetu yote yanakuwa safi. Hii ni pamoja na madawati na meza, simuna komputa za mezani. Vyote vita safishwa na kufutwa kwa dawa mara kwa mara.

*         Tutapunguza kutumia usafiri wa umma kwa wafanyakazi,pia kufanya kazi tukiwa majumabani itakuwa njia mbadala. Gari za shirika zitatumika kwa usafiri, kama haitawezekana, safari zisizozalazima zitaahirishwa au kufutwa.

*         Epuka au ahirisha shughuli zinazo husisha watu wengi mfano mikutano na mashirika wenza.

*         Fuatilia mwenendo wa ugonjwa katika maeneo yanayo kuzunguka. Chanzo cha taarifa iwe wizara ya afya au shirika la afya duniani (WHO) kwa anuani hii https://www.who.int/emergencies/diseases/novel-coronavirus-2019 . Usiamini sana taarifa kutoka mitandao ya jamii.


Kent Larsson
Country Manager
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Vi Agroforestry/Vi-Skogen
Country Office Tanzania
P.O. Box 621, Mwanza, Tanzania

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kauli mbiu yetu

BUFADESO kwa maendeleo ya wakulima

MUHIMU

Makala na picha zinazochapishwa katika blogu hii ni kwa ajili ya taarifa na kumbukumbu za Shirika la Bunda Farmers Development Support Organization (BUFADESO)
Hairuhusiwi kutumia yaliyomo katika blogu hii (HASA PICHA) kwa shughuli zozote bila ruhusa ya mmiliki wa blogu hii ambaye ni BUFADESO