Alhamisi, 5 Mei 2016

WAWEZESHAJI JAMII

Shirika la BUNDA FARMER`S DEVELOPMENT SUPPORT ORGANIZATION (BUFADESO) linalenga kufanikisha utekelezaji wa miradi na shughuli endelevu. Ili kufanikisha uendelevu wa shughuli za shirika na miradi ya walengwa yaani jamii, BUFADESO inatumia WAWEZESHAJI JAMII kufundisha, kuelekeza, Kuunganisha na kuwezesha wanachama wa shirika na jamii kwa ujumla.
Wawezeshaji Jamii wa BUFADESO wakiwa na Mratibu wa Shirika Ndg. Baraka Kamese

WAWEZESHAJI JAMII wa shirika la BUFADESO ni wakulima na wafugaji wataalam ambao ni wanachama wa shirika. Wawezeshaji Jamii hawa wamejengewa uwezo na Shirika la Vi AGROFORESTRY na kuhitimu mafunzo ya aina mbalimbali ikiwemo mafunzo ya Uimarishaji wa vikundi, Kilimo na Mabadiriko ya Tabia Nchi, Kilimo Biashara na Ujasiliamali na Masuala Mtambuka kama Usawa wa kijinsia na Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI.

Wawezeshaji jamii wa shirika la BUFADESO wanafanya kazi kwa kujitolea katika kata na vijiji wanavyotoka. Kila kata mwanachama wa Shirika la Bufadeso ina wawezeshaji jamii wawili; mwanaume na mwanamke.
Afisa kutoka Vi AGROFORESTRY Bw. Paschal Paul akitoa somo kwa wawezeshaji jamii wa shirika la BUFADESO

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kauli mbiu yetu

BUFADESO kwa maendeleo ya wakulima

MUHIMU

Makala na picha zinazochapishwa katika blogu hii ni kwa ajili ya taarifa na kumbukumbu za Shirika la Bunda Farmers Development Support Organization (BUFADESO)
Hairuhusiwi kutumia yaliyomo katika blogu hii (HASA PICHA) kwa shughuli zozote bila ruhusa ya mmiliki wa blogu hii ambaye ni BUFADESO