Alhamisi, 15 Julai 2021

FAIDA ZA VIKUNDI VYA KIJAMII VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA

 BUFADESO kupitia mradi wa ALIVE imekua ikifanya uhamasishaji wa mifumo ya kifedha vijijini (kuweka na kukopa) Hisa kupitia vikundi vya kijamii vya Huduma Ndogo za Fehda. Kupitia program hii watu mbalimbali wamekua wakinufaika hasa wanawake, Pichani ni Mama, Miriam Samsoni 55, Mama huyu ameweza kuweka umeme na kujenga nyumba kupitia fedha alizopata baada ya kumaliza mzunguko wa Hisa Mwanzoni mwa mwaka huu 2021 sio hivyo tu Bali amekua akisomesha watoto kupitia fedha anazokopa kwa riba nafuu kupitia kikundi chake Cha Kijamii cha Huduma Ndogo za Kifedha cha Umoja kinachopatika kata ya Sazira, Bunda.

Jumatatu, 9 Novemba 2020

Annual Agroforestry Symposium 2020



Vi Agroforestry’sAnnual Agroforestry Symposium will take place on Thurs 19th November to Sat 21st November at the Agriculture Training Centre in Bweri, Musoma.

·         This year’s theme will focus on Agroforestry for Food and Income security

·         Our guest speaker will be the Permanent Secretary for the Ministry of Agriculture, Mr Gerald Kusaya.

 

Vi Agroforestry warmly welcomes you to the Annual Agroforestry Symposium taking place from Thursday 19th November to Saturday 21st November 2020 between 9:00am to 5:00pm every day. The event will be hosted alongside our partners BUFADESO at the Agricultural Training Centre in Bweri, Musoma Municipal Council. The event aims to present information on the theme of Agroforestry for Food and Income Security.

                                                                                                        

We invite smallholder farmers and stakeholders from the agriculture sector, seed companies, pesticide companies, financial sector, manufacturing companies, university and tertiary institutions, textile companies, ministries and parastatals, research bodies and health and insurance companies among others to participate and showcase their products and services.

 

The Symposium will offer many learning opportunities through speeches, exhibitions, live demonstrations, networking, product stalls and learning sessions. We hope that farmers and other participants will be empowered with this knowledge and gain skills and contacts that will see them improve their livelihoods. Our guest speaker the Permanent Secretary for the Ministry of Agriculture, Mr Gerald Kusaya, will be there to share insight into the use of Agroforestry for Food and Income Security.

 

This will be an action packed 3 days, full of learning, competitions, and entertainment.Karibuni Sana.

---

 

Vi Agroforestry is a Swedish development organisation fighting poverty and climate change through Agroforestry and Sustainable Agricultural Land Management in Tanzania, Kenya, Rwanda and Uganda. Since its inception in 1983, Vi Agroforestry has contributed to the planting of over 134 million trees and has helped more than 2.4 million people out of poverty over the past 10 years.

 

Vi Agroforestry maintains its country office in Mwanza and runs programme interventions in 8 regions of Tanzania including Mwanza, Mara, Kagera, Dodoma, Mbeya, Songwe, Ruvuma, and Dar es Salaam. The Organization is committed to support small scale farmers to practise agroforestry and sustainable agriculture in Tanzania.

For more information, please visit www.viagroforestry.org   

Jumatano, 3 Juni 2020

SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI 2020


Siku ya Mazingira Duniani huadhimishwa kila tarehe 5 ya mwezi wa sita. Mwaka huu inaadhimishwa Siku ya Ijumaa, tarehe 5 Juni 2020 nchini Colombia. Dhima ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka huu italenga "Bioanuai" ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema "CELEBRATE BIODIVERSITY" kwa tafsiri rahisi "SHEREHEKEA BIOANUAI". Progamu ya Mazingira ya Umoja wa Mataifa; UNEP (UN Environmental Programme) imetangaza kuwa Colombia itakuwa mwenyeji wa Siku ya Mazingira Duniani Mwaka huu kwa kushirikiana na Ujerumani. Siku ya mazingira duniani huadhimishwa na nchi zaidi ya 143, Tanzania ikiwemo. Siku hii pia huitwa "Siku ya Watu"; kuonesha jinsi watu wanavyojali dunia na kusaidia utunzaji wa mazingira ya dunia.

Kwa nini Kauli Mbiu ya Mwaka huu inasema "SHEREHEKEA BIOANUANI" na kwa nini COLOMBIA awe mwenyeji wa mwaka huu?

Kwanza kabisa ni vizuri tukajua maana ya neno Bioanuai

Bioanuani ni mchanganyiko na uwiano wa viumbe hai; wanyama na mimea; vinavyoishi duniani. Bio maana yake ni maisha, na anuwai ni aina, kwa hiyo, bioanuwai ina maana ya aina ya maisha. Inajumuisha vitu vyote vinavyoishi duniani na katika bahari, kuanzia nyangumi wakubwa kabisa mpaka bacteria wadogo kabisa. Mahali ambapo aina nyingi tofauti, au ‘spishi’, au vitu vyenye uhai hukua pamoja, kama vile mwamba wa matumbawe au msitu, panasemekana kuwa na bioanuwai nyingi, na mahali ambapo pana spishi chache, kama shamba lililolimwa, au maeneo ya mjini, pana bioanuwai wachache.


Kauli mbiu inasema tusheherekee bioanui kwa sababu duniani kuna zaidi ya spishi za wanyama na mimea zaidi ya milioni moja. Lakini kutokana na changamoto za kidunia zilizopo sasa, kuna matishio makubwa ya viumbe mbalimbali kutoweka duniani imeonekana kwa sasa una umuhimu zaidi kutilia mkazo katika kulinda bioanuai. Nchi ya Colombia imechaguliwa kuwa mwenyeji wa mwaka huu wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira duniani kutokana na uwepo wa wanyama na mimea kwa wingi zaidi katika nchi hii. Nchi ya Colombia ina zaidi ya 10% ya bioanuani zilizopo duniani. Kitakwimu, nchi hiyo ndio inayoongoza (nchi ya kwanza) kwa kuwa aina nyingi ya ndege na pia ni nchi ya pili kwa kuwa na aina nyingi za mimea mbalimbali, vipepeo na samaki wa maji baridi. Pia nchi ya Colombia ni sehemu ya msitu mkubwa duniani uitwao Msitu wa Amazon.

Imeandaliwa na
Baraka Kamese
Mratibu BUFADESO

Kauli mbiu yetu

BUFADESO kwa maendeleo ya wakulima

MUHIMU

Makala na picha zinazochapishwa katika blogu hii ni kwa ajili ya taarifa na kumbukumbu za Shirika la Bunda Farmers Development Support Organization (BUFADESO)
Hairuhusiwi kutumia yaliyomo katika blogu hii (HASA PICHA) kwa shughuli zozote bila ruhusa ya mmiliki wa blogu hii ambaye ni BUFADESO