Jumanne, 12 Septemba 2017

TOZO NA ADA ZILIZOONDOLEWA NA WIZARA YA KILIMO


Chati ifuatayo inaonyesha ada na tozo mbalimbali zilizosamehewa na serikali kupitia Wizara ya Kilimo katika maeneo ya Mazao,  Ushirika, Mifugo na Uvuvi.  Hii ni fursa kwa wakulima, wavuvi na wafugaji kutumia vizuri nafasi ya misamaha hii kuongeza uzalishaji, usindikaji na biashara kwa ujumla. 


Tasnia
Eneo
Idadi ya Ada na Tozo zilizoondolewa
Eneo husika
Mazao
Kahawa
17
Ada kwa ajili ya leseni za: kuuza kahawa ya kijani kwa makampuni na vyama, kuendesha maghala, kuuza premium coffee kwa vyama na makampuni, kukoboa kahawa, kununua kahawa, uendeshaji wa minada

Tozo kwa ajili ya fomu za kuomba:
Kuendesha maghala, kukoboa kahawa, kuuza kahawa (premium), kuuza kahawa ya kijani, kusindika kahawa, kununua kaha
Sukari
16
Ada za kibali cha kuingiza sukari ya viwandani na ile ya kuziba pengo (Sugar Gap), ada ya usajili wa wafanyabiashara wa sukari ya kawaida na viwandani (wakubwa , wadogo na wakati), ada ya kibali cha uingizaji wa sukari ya viwandani nay a kawaida, ada ya leseni mbalimbali kwa uzalishaji wa sukari hapa nchini, ada ya marudio ya leseni mbalimbali kwa wazalishaji wa sukari na ada mbalimbali za leseni ya kuchakata miwa.
Tumbaku
10
Tozo ya Baraza la Tumbaku, ada ya leseni ya kuuza tumbaku nje, leseni ya kununua tumbaku mbichi, Kodi ya leseni ya kununua Tumbaku, Dhamana ya Benk Kuu (1%),  ada ya form ya maombi, Mchango wa ushirika wa mkoa, mchango wa chama cha msingi, gharama za masoko.
Mbegu
7
Tozo kwa ajili ya:- usajili wa muuza mbegu, fomu ya majaribio ya DUS,
fomu ya majaribio ya NPT, Ukaguzi mashambani, Majaribio ya mbegu, kibali cha kusafirisha mbegu, Tangazo la kusafirisha au kuagiza mbegu.
Mbolea
4
Tozo kwa ajili ya Usajili wa mfanyabiashara,
Ada ya leseni, Tozo kwa ajili ya Usajili wa mzalishaji wa mbolea,
Ada kwajili ya Usajili Mbolea
Korosho
2
Ada ya leseni ya kununulia korosho,
Gharama za magunia na Kamba
Pamba
2
Tozo ya kituo cha kununulia pamba, tozo ya maendeleo ya elimu
Chai
1
Gharama za uendeshaji wa vyama vya wakulima (sh 5 kwa kilo)
Mfuko wa Pembejeo
1
Ada ya nyaraka za kuombea mkopo ambayo ni 1% ya mkopo
Ushirika
Ushirika
20
Aina 5 za Ada ya usajili wa mabadiliko ya masharti ya vyama vya  Msingi, Pili, Kati, Shirikisho na vyama vya Ushirika kwa ajili ya uwekezaji wa pamoja.

Aina 5 za Ada ya uchunguzi  kwenye Rejista ya vyama vya  Msingi, Pili, Kati, Shirikisho na vyama vya Ushirika kwa ajili ya uwekezaji wa pamoja.

Aina 5 za Ada ya uchunguzi  kwenye Rejista ya vyama vya  Msingi, Pili, Kati, Shirikisho na vyama vya Ushirika kwa ajili ya uwekezaji wa pamoja.

Aina 5 za Ada ya uchunguzi  wa taarifa za vyama vya  Msingi, Pili, Kati, Shirikisho na vyama vya Ushirika kwa ajili ya uwekezaji wa pamoja.

Aina 5 za Ada kwa ajili ya utoaji wa nakala za nyaraka   za vyama vya  Msingi, Pili, Kati, Shirikisho na vyama vya Ushirika kwa ajili ya uwekezaji wa pamoja.  
Mifugo

Maziwa
4
Ada ya usajili wa wadau, Ukusanyaji wa maziwa, usambazaji wa maziwa, Export permit
Nyama
4
Usajili wa wafugaji, usajili wa minada, Export clearance Certificates, Ada ya usajili wa wafanyabiashara wa mifugo na nyama
Huduma za Afya
17
Tozo ya Kibali cha kuingiza ngozi za ng’ombe, Tozo ya Kibali cha kuingiza ngozi za mbuzi/kondoo,  tozo ya kibali cha afya cha kusafirisha Ng’ombe, tozo ya kibali cha afya cha kusafirisha Mbuzi au Kondoo, tozo ya kibali cha afya cha kusafirisha punda au farasi, tozo ya kibali cha kusafirisha ngamia,nguruwe, vifaranga, mayai (Fertilized), mayai ya kula, kuku/kanga, nyama pori, ndege pori, maziwa, mbwa na paka
Uvuvi

Export Royalty
1
Export Royalty
Maendeleo ya uvuvi
4
Movement Permit, ada yaukaguzi wa kiwanda au ghala, Tozo ya cheti cha afya, ada ya usajili wa chombo
Jumla
110


Chanzo ACT

Jumatano, 9 Agosti 2017

TAARIFA KUTOKA WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO.

TAARIFA KWA UMMA
Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali anatarajia kuhakiki Mashirika yote Yasiyo ya Kiserikali kuanzia tarehe 21 hadi 31 Agosti, 2017. Lengo kuu la zoezi hili ni Kuhuisha orodha ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini, Kuboresha Kanzi Data ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na kupima utekelezaji wa majukumu ya Mashirika haya. Zoezi hili litafanyika katika Kanda tano (5). Kanda ya Mashariki itahudumia mikoa ya DAR ES SALAAM, LINDI, MTWARA, PWANI na MOROGORO na Kituo kitakuwa Idara ya Uratibu wa NGOs DAR ES SALAAM; Kanda ya Kati itahudumia mikoa ya DODOMA, SINGIDA, TABORA na KIGOMA na Kituo kitakuwa DODOMA, Makao Makuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto iliyopo Chuo Kikuu cha Dodoma, Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Maendeleo ya Jamii, Jengo Na. 11, Dodoma; Kanda ya Kaskazini itahudumia mikoa ya KILIMANJARO, TANGA, ARUSHA na MANYARA na Kituo kitakuwa katika Ofisi ya Katibu Tawala (M) KILIMANJARO; Kanda ya Ziwa itahudumia mikoa ya MWANZA, KAGERA, MARA, GEITA, SIMIYU na SHINYANGA na Kituo kitakuwa katika Ofisi ya Katibu Tawala (M) MWANZA na Kanda ya Nyanda za Juu - Kusini itahudumia mikoa ya MBEYA, RUVUMA, KATAVI, RUKWA, SONGWE, NJOMBE na IRINGA na Kituo kitakuwa katika Ofisi ya Katibu Tawala (M), MBEYA. Wakati wa uhakiki kila shirika linapaswa kuwasilisha Cheti Halisi cha Usajili, Nakala ya Cheti cha Usajili, kujaza fomu ya uhakiki NGO-Fomu/UHK/2017 inayopatikana katika Tovuti (www.tnnc.go.tz), Stakabadhi za Malipo ya Ada ya mwaka toka kuanzishwa kwa shirika, Barua kutoka kwa Afisa Maendeleo ya Jamii (Mkoa/Wilaya/Halmashauri/Manispaa) ikithibitisha uwepo wa Ofisi ya Shirika na nakala ya katiba iliyothibitishwa na Msajili wa NGOs. Aidha, Mashirika yote yatakayoshindwa kuhakikiwa katika vituo vya Kanda tajwa hapo juu, yatafutiwa Usajili na kuondolewa kwenye Regista ya Msajili wa NGOs. Ili kutoa fursa ya kuhuisha Kanzi Data na Benki ya Takwimu, Usajili wa NGOs utasitishwa kuanzia tarehe 21 Agosti hadi 30 Novemba, 2017.

 M.S. Katemba
MSAJILI WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI

Kauli mbiu yetu

BUFADESO kwa maendeleo ya wakulima

MUHIMU

Makala na picha zinazochapishwa katika blogu hii ni kwa ajili ya taarifa na kumbukumbu za Shirika la Bunda Farmers Development Support Organization (BUFADESO)
Hairuhusiwi kutumia yaliyomo katika blogu hii (HASA PICHA) kwa shughuli zozote bila ruhusa ya mmiliki wa blogu hii ambaye ni BUFADESO