Jumanne, 14 Juni 2016
Jumamosi, 14 Mei 2016
MKUTANO MKUU WA MWAKA ULIOFANYIKA TAREHE 14/05/2016
Wajumbe wa mkutano Mkuu wa Mwaka katika eneo la Mkutano Shule ya Sekondari Sazira
Viongozi wa Shirika la BUFADESO
Wasimamizi wa Uchaguzi wakihesabu kura za wagombea nafasi za uongozi wa Shirika.
Msimamizi wa Uchaguzi akitangaza matokeo ya kura zilizopigwa
Wajumbe wa katika Kikao
Mratibu wa Shirika Ndg. Baraka Kamese akitoa maelezo ya mikakati ya shirika
Mkutano mkuu wa shirika la BUFADESO kwa mwaka huu umefanyika leo siku ya Jumamosi tarehe 14/05/2016 katika Shule ya msingi Sazira. Katika Mkutano Mkuu huu viongozi wapya wa shirika la BUFADESO wataoongoza shirika kwa miaka mitatu ijayo wamechaguliwa. Vingozi waliochaguliwa kuongoza shirika ni Edward Chacha kutoka kata ya Mcharo- MWENYEKITI WA SHIRIKA, Anifa Malegesi kutoka Neruma - MAKAMU MWENYEKITI, Joseph Itoka wa kata ya Wariku - KATIBU MKUU, Juma Salumu kutoka kata ya GuTA - KATIBU MSAIDIZI na Marwa Nyamhanga - MHAZINI WA SHIRIKA.
Alhamisi, 5 Mei 2016
WAWEZESHAJI JAMII
Shirika
la BUNDA FARMER`S DEVELOPMENT SUPPORT ORGANIZATION (BUFADESO) linalenga
kufanikisha utekelezaji wa miradi na shughuli endelevu. Ili kufanikisha
uendelevu wa shughuli za shirika na miradi ya walengwa yaani jamii, BUFADESO
inatumia WAWEZESHAJI JAMII kufundisha, kuelekeza, Kuunganisha na kuwezesha
wanachama wa shirika na jamii kwa ujumla.
Wawezeshaji Jamii wa BUFADESO wakiwa na Mratibu wa Shirika Ndg. Baraka Kamese
WAWEZESHAJI
JAMII wa shirika la BUFADESO ni wakulima na wafugaji wataalam ambao ni
wanachama wa shirika. Wawezeshaji Jamii hawa wamejengewa uwezo na Shirika la Vi
AGROFORESTRY na kuhitimu mafunzo ya aina mbalimbali ikiwemo mafunzo ya Uimarishaji
wa vikundi, Kilimo na Mabadiriko ya Tabia Nchi, Kilimo Biashara na Ujasiliamali
na Masuala Mtambuka kama Usawa wa kijinsia na Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI.
Wawezeshaji
jamii wa shirika la BUFADESO wanafanya kazi kwa kujitolea katika kata na vijiji
wanavyotoka. Kila kata mwanachama wa Shirika la Bufadeso ina wawezeshaji jamii
wawili; mwanaume na mwanamke.
Afisa kutoka Vi AGROFORESTRY Bw. Paschal Paul akitoa somo kwa wawezeshaji jamii wa shirika la BUFADESO
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)
Kauli mbiu yetu
BUFADESO kwa maendeleo ya wakulima
MUHIMU
Makala na picha zinazochapishwa katika blogu hii ni kwa ajili ya taarifa na kumbukumbu za Shirika la Bunda Farmers Development Support Organization (BUFADESO)
Hairuhusiwi kutumia yaliyomo katika blogu hii (HASA PICHA) kwa shughuli zozote bila ruhusa ya mmiliki wa blogu hii ambaye ni BUFADESO
